Imeelezwa   kuwa  
shughuli za  ajira muda
zilizofanywa na walegwa wa mpango wa kaya maskini TASAF awamu ya tatu kama
kutunza Misitu ya asili,uvunaji wa maji ya mvua, na utunzaji wa udongo,ikitumika
inavyopaswa itaweza kuleta mabadiliko 
chanya kwa  jamii  na kuweza kujiletea maendeleo endelevu.
Kauli hiyo imetolewa na
Mratibu wa Tassaf wa halmasahauri ya wilaya ya Mpwapwa Bwana Paskal Jeremia  alipokuwa akiongea  na waandishi wa habari ofisini kwake juu
tadhimini  ya utekelezaji wa mpango wa
ajira za muda zijulikanozo kama (PWP)kwa wanufaika wa mpango huo wilayani hapa
Jeremia amesema  rasilimali hizo kama ujengaji wa miundo mbinu
ya  kuvuna maji ya mvua, wa  utunzaji wa misitu, na  uhifadhi wa 
udongo  ngazi ya jamii italeta mabadiliko  kuwa  mazuri  zaidi 
na jamii kuweza kujiletea 
maendelea endelevu katika maeneo yao yanayoishi. 
Aidha  amesema kwa sasa zoezi hilo limetekelezwa kwa
zaidi ya asilimia 70% katika vijiji vyote 
ambavyo  mradi huo ulitekelezwa
bali amesema kuna baadhi ya changamotozilizojitokeza kama za malipo ambazo
makao makuu yanazifanyia kazi na walegwa watalipwa muda si mrefu.
 Amesema 
Mpango wa Tassaf  katika awamu
zote tatu umeweza kuonyesha mafanikio 
mazuri ngazi ya jamii na halmashauri 
kwa walegwa walioko kwenye mpango wameweza  kubadilisha maisha yao kwa kujiibulia miradai
midogomidogo na kuweza kumubudu maisha yao ya kila siku.
Kwa upande  wake ofisa 
ushauri naufuatiliaji wa Tassaf  wilayani hapa bwana Hosea Sichone amesema  madhumuni ya 
mpango  ni kuziwezesha kaya
maskini  sana kuongeza matumizi muhimu
kwa jia endelevu  na kuziwezesha kaya
hizo kuwa na pesa za matumizi wakati 
kipindi kigumu zaidi.
Hata hivyo Hosea amesema
kuwa  pia madhumuni mengine  ni kuwekeza katika rasilimali watu  hasa watoto ikiwa na lengo la kuaandaa kizazi
chenye tija ,kuimarisha  shughuli za
kuongeza kipato na kuongeza shughuliza za huduma za jamii.
Mmmoja wawanufaika wa
Mpango huo Bi Maligalitha Chinoga  amesema kuwa 
miradi ya kutoa ajira za muda kwa 
kaya maskini  japo kuwa unalenga
katika utunzaji wa mazingira na mabadiliko ya hali hewa lakini lakini uharibifu
mkubwa wa mazingira katika wilaya yetu unatishia uendelevu wa miradi hiyo.
Comments
Post a Comment