CHAMA CHA WALIMU CHAIDAI SERIKALI MILION 412.7 MPWAPWA
Na noel Stephen - Mpwapwa CHAMA cha walimu wilayani mpwapwa mkoani Dodoma kinaidai serikali kiasi cha tsh milioni 412,701,983 kama madeni ya mapunjo ya mishara, pesa za likizo na upandishwaji wa madaraja. Kwa walimu wake kwa kipindi cha kuanzia desemba 2012 na hadi feb 2014. Kauli hiyo imelotelewa na katibu wa chama hicho wilayani hapa Donard Kisamaba alipokuwa akisoma taarifa ya utekelezaji katika mkutano mkuu wa mwaka wa chama hicho uliofanyika katika ukumbi wa ccm mjini mpwapwa. Kisamba alisema kuwa madeni hayo ni mapunjo ya mishahara na makato mbalimbali ambayo walimu wanamdai mwajili kama haki zao za msingi kazini . ALISEMA serikali ikiwa katika mchakato wa matokeo makubwasasa (big result now) katika idara ya elimu hayatapatikana ka...