Posts

Showing posts from February, 2020

Madiwani wa wakumbushwa kujaza tamko la mali pindi udiwani unapokoma.

Image
Mpwapwa.   Waheshimiwa Madiwani wa Halmashauri yua Wilaya ya Mpwapwa Mkoani Dodoma, wamekumbushwa kujaza za maadili na kuwasilisha Matamko   ya Mali yao na Madeni katika Ofisi za Sekretarieti ya Maadili ya Viongozi wa Umma pindi Udiwani wao unapokoma mwezi Julai 2020. Hayo yalisemwa na Afisa wa Sekretarieti ya Maadili ya Viongozi wa Umma Bw. George Shilla wakati akiwasilisha mada ya Tamko la Mali na Madeni katika kikao cha Baraza la Madiwani la Halimashauri ya Wilaya ya Mpwapwa juzi. “Jukumu la kujaza   fomu ya maadili   ni jukumu la kila kiongozi wa umma   na halimuhusu mwajiri wake au mkuu wake wa idara hivyo kujaza fomu hizi ni takwa la   kisheria     ya Maadili namba 13 ya Mwaka 1995 inayomtambua Kiongozi wa Umma binafsi kila mmoja na sio hiyari ya kiongozi” alifafanua bwana Shilla. Aidha Bw. Shilla alidai kuwa     Madiwani wana wajibu wao wa kuwasilisha fomu hizo kwa Kamishna wa Maadili   wenyewe na siyo kutegemewa kuwasilishiwa na Mkurugenzi wa halmashauri

WAZIRI WA MAMNBO YA NDANI YA NCHI ATANGAZA NEEMA KWA BODABODA.

Image
MPWAPWA. WAZIRI wa mambo ya ndani ya nchi Mhe George Simbachawene   amepiga marufuku kwa polisi kukamata wananchi,bodaboda       na kuwanyanyasa   na pia amepiga marufuku   kufanya oparesheni yoyote ndani ya mkoa au wilaya   bila kuwashirikisha wenyeviti wa kamati za ulinzi na usalama. Simbachawene ametoa kauli hiyo wilayani Mpwapwa alipokuwa kwenye ziara ya siku moja alipokuwa akizungumza na madiwani wa halmasahauri ya wilaya ya Mpwapwa. Simbachawene amesema kuna baadhi ya polisi wamekuwa wakikiuka   taratibu   na kanuni za kipolisi kwa kuwakamata wananchi na hasa madreva wa pikipiki   maarufu kama bodaboda   kwa kisingizio kama mimi nimewatuma “ kuanzia leo kupitia hapa Mpwapwa natangaza bodaboda wasisumbuliwe na   kukamatwakamatwa pasipo kuwa na sababu za msingi” alizungumza . Pia amewataka bodaboda wote nchi kuweza   kuzingatia sheria za usalama barabarani   ili kuweza kupunguza ajari na kuweza kuokoa maisha ya wao wenyewe na abiria wao. Akizungumza na
Image
MPWAPWA -MICHEZO Walimu wa michezo Nchini wametakiwa  kutoa fursa sawa kwa vijana wenye viapaji  wa mjini na vijijini ili kuweza kufikia ndoto zao kimchezo kama walizofikia wachezaji wakubwa wa kimataifa. Kauli hiyo ilitolewa na ofisa Elimu Sekondari  wilaya  ya Mpwapwa bwana Nelson Milanzi  katika zoezi la kufunga kozi ya siku tatu kwa walimu wa wa michezo wa wilaya ya Mpwapwa. Mwalimu Milanzi  alisema michezo ikiwekwezwa vizuri kwa watoto  vijana inaweza ikapunguza changamoto  ya ajira kwa  kwa vijana  katika taifa letu “hasa kwa wale wenye vipaji  hasa wale walioko pembezoni kwa mfano akina Mbwana Samata  waliotokea mbagala huko mbona hutuwasikii vijana wenye vipaji wanaotoka vijijini  inaamana hawako wenye vipaji huko sasa nyie nendeni mkawatengeneze akina Samata wengi ” Naye  mkufunzi wa kozi hiyo Bwana Charles Maguzu  aliwataka Walimu wa michezo  katika shule   za msingi na sekondari  kuanza kuipa kiapumbele  michezo katika shule zao kwa lengo la k