Posts

Showing posts from December, 2016

POLISI MPWAPWA YAKABILIWA NA UHABA VITENDEA KAZI.

Image
Na Stephen noel mpwapwa. JESHI la polisi wilayani Mpwapwa mkoani Dodoma linakabiliwa na upungufu  mkubwa wa vityendea kazi ikiwemo magari na pikipiki kitu kinachopelekea jeshi hilo kushidwa kuwahi katika  matukio ya kiuharifu. Kauli hiyo  ilitolewa jana na Mrakibu wa polisi   bwana Paulo Ngonyani mkuu wa kitengo cha Intelinjesia mkoani Dodoma  alipokuwa  katika hafla ya kukabithiwa Pikipiki mbili zilizonunuliwa na wadau wa polisi wa wilayani  Mpwapwa kwa lengo la kupambana  na uharifu wilayani hapa. Bwana Ngonyani alisema katika jeshi la polisi limekuwa likilalamikiwa sana na wanajmii kuwa wamekuwa wakichelewa kufika katika matukio ya kiuharifu kutokana na kukabiliwa na chanagamoto kubwa ya ukosefu wa vitendea kazi kama vyombo vya usafiri,pamoja na mafuta Aidha Ngonyani  alisema  kwamba  ili kuimarisha dhana ya polisi jamii wameamua kuwashirikisha wadau  wa maendeleo katika wilaya husika kuweza kusaidiana kuzikabili changamoto zinazo likabili jeshi
Imeelezwa    kuwa    shughuli za   ajira muda zilizofanywa na walegwa wa mpango wa kaya maskini TASAF awamu ya tatu kama kutunza Misitu ya asili,uvunaji wa maji ya mvua, na utunzaji wa udongo,ikitumika inavyopaswa itaweza kuleta mabadiliko   chanya kwa   jamii   na kuweza kujiletea maendeleo endelevu. Kauli hiyo imetolewa na Mratibu wa Tassaf wa halmasahauri ya wilaya ya Mpwapwa Bwana Paskal Jeremia   alipokuwa akiongea   na waandishi wa habari ofisini kwake juu tadhimini   ya utekelezaji wa mpango wa ajira za muda zijulikanozo kama (PWP)kwa wanufaika wa mpango huo wilayani hapa Jeremia amesema   rasilimali hizo kama ujengaji wa miundo mbinu ya   kuvuna maji ya mvua, wa   utunzaji wa misitu, na   uhifadhi wa   udongo   ngazi ya jamii italeta mabadiliko   kuwa   mazuri   zaidi   na jamii kuweza kujiletea   maendelea endelevu katika maeneo yao yanayoishi. Aidha   amesema kwa sasa zoezi hilo limetekelezwa kwa zaidi ya asilimia 70% katika vijiji vyote   ambavyo   mradi huo ul

LITA MPWAPWA YAPATA MAABARA YA KISASA

Image
Dkt MACIEJ KLOCKIEWICS akiwa katika hafla ya uzinduzi wa maabara ya kisasa MPWAPWA Dkt Justina kutoka Uholanzi katika hafla ya ufunguzi wa maabara ya kisasa LITA MPWAPWA. Dkt Justina akicheza SHOO  na BAADHI YA Wanachuo wa LITA mpwapwa wakifurahia UFUNGUZI w maabara ya uchunguzi wa magonjwa ya mifugo   lita Mpwapwa. Mkuu wa wilaya ya mpwapwa akiongea neno ktika uzinduzi wa hafla hiyo. Dkt Mery Mashingo akiwa katika picha y pamoja na wgeni waalikwa na wafadhili wa maabar hiyo kutoka nchi ya Uholanzi. Dkt Mery Mashingo akifungua maabara ya uchunguzi wa magonjwa ya wanyama yatokanayo na wadudu iliyo fadhiliwa na chuo kikuu cha sayansi cha nchini uholanzi, katika tasisi ya uwakala wa mafunzo ya mifugo LITA kampasi ya Mpwapwa.